TECNO NA MAN CITY KUKUZA VIPAJI VYA MPIRA TANZANIA.



Kampuni ya simu ya Tecno Mobile iliyoingia makubaliano ya kibiashara na Timu maarufu inayoshiriki  ligi kuu ya mpira wa miguu nchini Uingereza Klabu ya Manchester City, kwa pamoja wamekuja na mikakati ya kukuza soka nchini Tanzania.
Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa  na Afisa  Mahusiano wa kampuni hiyo Bwana Eric Mkomoye, amesema kua pamoja na kuwapo kwa fursa za kibiashara zilizopo kati ya klabu ya Manchester City na Tecno Mobile lakin pia Tecno wamedhamiria kutumia fursa hiyo kukuza viwango vya mpira kwa watoto wa kitanzania ambao wazazi wao pia ni wateja wa kampuni hiyo


“Tutawapa watoto wa kitanzania kadhaa nafasi ya kwenda Manchester city kufanya training kule na pia wakifanya vizuri wanauwezo wa kuchukuliwa kwa academy ya Manchester City , huko watakutana watoto wengine tokea nchi ambazo Tecno Mobile  inafanya kazi zake  kama Kenya, Uganda, Ghana na Misri na kwa kuanza tutapeleka watoto wawili”


Katika ushirikiano huu pia imeleta simu maalumu itakayotumika alama maalumu ya Tecno  Mobile na klabu ya Manchester City, Eric alifafanua.
“Tumeleta Tecno Camon CX Manchester city limited version, ni simu maalumu inayoonesha ushirikiano wetu na Man city pia  ni simu maalumu inayotumika wachezaji wa Manchester city katika  kupiga  picha , hivyo tumeileta sokoni maalumu kwa wateja wetu kipindi waweze kupata  experience wanayopata man city katika  simu hii.”



Aliongeza “Simu hii inakuja na box kubwa lenye zawadi maalumu kwa wateja kama chupa ya kimichezo, speaker, fimbo maalumu ya kupigia picha pamoja na kava maalumu.”
TECNO Mobile wameleta simu ikiwa ni toleo maalumu la tecno camon cx iliyokua sokoni mapema kidogo ila limeboreshwa Zaidi, hivyo inaenda na wakati uwezo wa kamera yake ni 16mp nyuma na mbele zinazosaidiwa na flashi mbili mbele nanne nyuma, uwezo wake ndani ni 64 GB huku ikisukuma data vizuri  kwa 4GB Ram,  




Watoto watakaochaguliwa  na Tecno Mobile kwenda katika trining hiyo wanatarajiwa kuondoka nchini mwisho wa mwezi nane, na vigezo vikubwa Tecno imetumia wataalamu wa soka nchini kutafuta vipaji hivi, Majina ya watoto hawa yatatangazwa kupitia mitandao  ya kijamii ya Tecno Mobile.




Post a Comment

0 Comments